ترجمة سورة الرحمن

Ali Muhsin Al - Swahili translation

ترجمة معاني سورة الرحمن باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation.

Ar-Rahman


Arrah'man, Mwingi wa Rehema

Amefundisha Qur'ani.

Amemuumba mwanaadamu,

Akamfundisha kubaini.

Jua na mwezi huenda kwa hisabu.

Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.

Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,

Ili msidhulumu katika mizani.

Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.

Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.

Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.

Na nafaka zenye makapi, na rehani.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..

Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Anaziendesha bahari mbili zikutane;

Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Kila kilioko juu yake kitatoweka.

Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.

Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Bustani zenye matawi yaliyo tanda.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Humo katika kila matunda zimo namna mbili.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.

Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Za kijani kibivu.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Na chemchem mbili zinazo furika.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Humo wamo wanawake wema wazuri.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
سورة الرحمن
معلومات السورة
الكتب
الفتاوى
الأقوال
التفسيرات

سورة (الرَّحْمن) من السُّوَر المكية، وقد أبانت عن مقصدٍ عظيم؛ وهو إثباتُ عموم الرحمة لله عز وجل، وقد ذكَّر اللهُ عبادَه بنِعَمه وآلائه التي لا تُحصَى عليهم، وفي ذلك دعوةٌ لاتباع الإله الحقِّ المستحِق للعبودية، وقد اشتملت السورةُ الكريمة على آياتِ ترهيب وتخويف من عقاب الله، كما اشتملت على آياتٍ تُطمِع في رحمةِ الله ورضوانه وجِنانه.

ترتيبها المصحفي
55
نوعها
مكية
ألفاظها
352
ترتيب نزولها
97
العد المدني الأول
77
العد المدني الأخير
77
العد البصري
76
العد الكوفي
78
العد الشامي
78

* سورة (الرَّحْمن):

سُمِّيت سورة (الرَّحْمن) بهذا الاسم؛ لافتتاحها باسم (الرَّحْمن)، وهو اسمٌ من أسماءِ الله تعالى.

* ذكَرتْ سورةُ (الرحمن) كثيرًا من فضائلِ الله على عباده:

عن جابرِ بن عبدِ اللهِ رضي الله عنهما، قال: «خرَجَ رسولُ اللهِ ﷺ على أصحابِه، فقرَأَ عليهم سورةَ الرَّحْمنِ، مِن أوَّلِها إلى آخِرِها، فسكَتوا، فقال: «لقد قرَأْتُها على الجِنِّ ليلةَ الجِنِّ فكانوا أحسَنَ مردودًا منكم! كنتُ كلَّما أتَيْتُ على قولِه: {فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ}، قالوا: لا بشيءٍ مِن نِعَمِك رَبَّنا نُكذِّبُ؛ فلك الحمدُ!»». أخرجه الترمذي (٣٢٩١).

1. من نِعَم الله الظاهرة (١-١٣).

2. نعمة الخَلْق (١٤-١٦).

3. نِعَم الله في الآفاق (١٧-٢٥).

4. من لطائف النِّعَم (٢٦-٣٢).

5. تحدٍّ وإعجاز (٣٣-٣٦).

6. عاقبة المجرمين (٣٧-٤٥).

7. نعيم المتقين (٤٦-٧٨).

ينظر: "التفسير الموضوعي لسور القرآن الكريم" لمجموعة من العلماء (7 /550).

مقصدُ سورة (الرَّحْمن) هو إثباتُ الرحمةِ العامة لله عز وجل، الظاهرةِ في إنعامه على خَلْقه، وأعظمُ هذه النِّعَم هو نزول القرآن، وما تبع ذلك من نِعَم كبيرة في هذا الكون.

يقول الزَّمَخْشريُّ: «عدَّد اللهُ عز وعلا آلاءه، فأراد أن يُقدِّم أولَ شيءٍ ما هو أسبَقُ قِدْمًا من ضروب آلائه وأصناف نَعْمائه؛ وهي نعمة الدِّين، فقدَّم من نعمة الدِّين ما هو في أعلى مراتبِها وأقصى مَراقيها؛ وهو إنعامُه بالقرآن وتنزيلُه وتعليمه؛ لأنه أعظَمُ وحيِ الله رتبةً، وأعلاه منزلةً، وأحسنه في أبواب الدِّين أثرًا، وهو سَنامُ الكتب السماوية ومِصْداقها والعِيارُ عليها.

وأخَّر ذِكْرَ خَلْقِ الإنسان عن ذكرِه، ثم أتبعه إياه؛ ليعلمَ أنه إنما خلَقه للدِّين، وليحيطَ علمًا بوحيِه وكتبِه وما خُلِق الإنسان من أجله، وكأنَّ الغرض في إنشائه كان مقدَّمًا عليه وسابقًا له، ثم ذكَر ما تميَّز به من سائر الحيوان من البيان؛ وهو المنطقُ الفصيح المُعرِب عما في الضمير». "الكشاف" للزمخشري (4 /443).