ترجمة سورة المرسلات

Ali Muhsin Al - Swahili translation

ترجمة معاني سورة المرسلات باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation.

Al-Mursalat


Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!

Na zinazo vuma kwa kasi!

Na zikaeneza maeneo yote!

Na zinazo farikisha zikatawanya!

Na zinazo peleka mawaidha!

Kwa kuudhuru au kuonya,

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!

Wakati nyota zitakapo futwa,

Na mbingu zitakapo pasuliwa,

Na milima itakapo peperushwa,

Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,

Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?

Kwa siku ya kupambanua!

Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?

Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!

Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?

Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?

Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?

Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?

Mpaka muda maalumu?

Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya

Walio hai na maiti?

Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!

Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!

Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.

Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!

Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,

Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.

Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,

Na matunda wanayo yapenda,

Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.

Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?
سورة المرسلات
معلومات السورة
الكتب
الفتاوى
الأقوال
التفسيرات

سورة (المُرسَلات) من السُّوَر المكية، نزلت بعد سورة (الهُمَزة)، وقد جاءت ببيانِ قدرة الله على بعثِ الناس بعد هلاكهم؛ فهو المتصفُ بالرُّبوبية والألوهية، وقد افتُتحت بمَشاهدِ القيامة، والتذكير بمَصارعِ الغابرين، وذكَرتْ تأمُّلات في خَلْقِ الإنسان والكون؛ ليعودَ الخلقُ إلى أوامرِ الله، وليستجيبوا له سبحانه، و(المُرسَلات): هي الرِّياحُ التي تهُبُّ متتابِعةً.

ترتيبها المصحفي
77
نوعها
مكية
ألفاظها
181
ترتيب نزولها
33
العد المدني الأول
50
العد المدني الأخير
50
العد البصري
50
العد الكوفي
50
العد الشامي
50

* سورة (المُرسَلات):

سُمِّيت سورة (المُرسَلات) بذلك؛ لافتتاحها بالقَسَمِ الإلهيِّ بـ(المُرسَلات)؛ وهي: الرِّياح التي تهُبُّ متتابِعةً.

سورة (المُرسَلات) من السُّوَر التي شيَّبتْ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم:

عن ابنِ عباسٍ رضي الله عنهما، قال: «قال أبو بكرٍ الصِّدِّيقُ رضي الله عنه لرسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم: يا رسولَ اللهِ، أراكَ قد شِبْتَ! قال: «شيَّبتْني هُودٌ، والواقعةُ، والمُرسَلاتُ، و{عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ}، و{إِذَا اْلشَّمْسُ كُوِّرَتْ}». أخرجه الحاكم (3314).

1. مَشاهد القيامة (١-١٥).

2. مَصارع الغابرين (١٦-١٩).

3. تأمُّلات في خَلْقِ الإنسان والكون (٢٠-٢٨).

4. عودٌ لمَشاهد القيامة (٢٩-٥٠).

ينظر: "التفسير الموضوعي لسور القرآن الكريم" لمجموعة من العلماء (8 /540).

مقصدُ سورة (المُرسَلات): الاستدلالُ على وقوع البعث بعد فَناء الدنيا، والاستدلال على إمكانِ إعادة الخَلْقِ بما سبَق من خَلْقِ الإنسان وخلق الأرض، وفي ذلك دلائلُ على قدرة الله، واتصافِه بالوَحْدانية والرُّبوبية.

ينظر: "التحرير والتنوير" لابن عاشور (29 /419).