ترجمة سورة المطفّفين

Ali Muhsin Al - Swahili translation

ترجمة معاني سورة المطفّفين باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation.

Al-Mutaffifin


Ole wao hao wapunjao!

Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.

Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa

Katika Siku iliyo kuu,

Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?

Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

Unajua nini Sijjin?

Kitabu kilicho andikwa.

Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!

Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.

Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.

Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!

Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.

Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.

Kisha wataingia Motoni!

Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.

Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.

Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?

Kitabu kilicho andikwa.

Wanakishuhudia walio karibishwa.

Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.

Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,

Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,

Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.

Na mchanganyiko wake ni Tasniim,

Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.

Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.

Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.

Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.

Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.

Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.

Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,

Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.

Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?
سورة المطففين
معلومات السورة
الكتب
الفتاوى
الأقوال
التفسيرات

سورة (المُطفِّفين) من السُّوَر المكية، وقد افتُتحت بوعيد المُطفِّفين الذين يتلاعبون بالميزان بُغْيةَ خداع الناس، متناسِين أنَّ هناك يومًا يبعثُ اللهُ فيه الخلائقَ، يحاسبهم على كلِّ صغيرة وكبيرة، وقد جاء فيها وعيدُ الفُجَّار بالعقاب الأليم، ووعدُ الأبرار بالثواب العظيم، وإكرامُ المؤمنين وإيلامُ المجرمين يوم البعث؛ جزاءً لهم على أعمالهم، وفي هذا كلِّه دعوةٌ للمُطفِّفين أن يؤُوبُوا إلى الله، ويَرجِعوا عن باطلهم.

ترتيبها المصحفي
83
نوعها
مكية
ألفاظها
170
ترتيب نزولها
86
العد المدني الأول
36
العد المدني الأخير
36
العد البصري
36
العد الكوفي
36
العد الشامي
36

* قوله تعالى: {وَيْلٞ لِّلْمُطَفِّفِينَ} [المطففين: 1]:

عن عبدِ اللهِ بن عباسٍ رضي الله عنهما، قال: «لمَّا قَدِمَ النبيُّ ﷺ المدينةَ، كانوا مِن أخبَثِ الناسِ كَيْلًا؛ فأنزَلَ اللهُ عز وجل: {وَيْلٞ لِّلْمُطَفِّفِينَ} [المطففين: 1]؛ فأحسَنوا الكَيْلَ بعد ذلك». أخرجه ابن حبان (٤٩١٩).

* سورة (المُطفِّفين):

سُمِّيت سورة (المُطفِّفين) بذلك؛ لافتتاحها بقوله تعالى: {وَيْلٞ لِّلْمُطَفِّفِينَ} [المطففين: 1]؛ وهم: الذين يتلاعبون في المكيال بُغْيةَ خداع الناس.

1. إعلان الحرب على المُطفِّفين (١-٦).

2. وعيد الفُجَّار بالعقاب الأليم (٧-١٧).

3. وعد الأبرار بالثواب العظيم (١٨-٢٨).

4. إكرام المؤمنين، وإيلام المجرمين (٢٩-٣٦).

ينظر: "التفسير الموضوعي لسور القرآن الكريم" لمجموعة من العلماء (9 /66).

يقول ابن عاشور: «اشتملت على التحذيرِ من التطفيف في الكيل والوزن، وتفظيعِه بأنه تحيُّلٌ على أكلِ مال الناس في حال المعاملة أخذًا وإعطاءً.
وأن ذلك مما سيُحاسَبون عليه يوم القيامة.
وتهويل ذلك اليوم بأنه وقوفٌ عند ربهم؛ ليَفصِلَ بينهم، وليجازيَهم على أعمالهم، وأن الأعمال مُحصاةٌ عند الله.
ووعيد الذين يُكذِّبون بيوم الجزاء، والذين يُكذِّبون بأن القرآن منزل من عند الله.

وقوبل حالُهم بضدِّه من حال الأبرار أهلِ الإيمان، ورفعِ درجاتهم، وإعلان كرامتهم بين الملائكة والمقربين، وذكرِ صُوَرٍ من نعيمهم.
وانتقل من ذلك إلى وصف حال الفريقين في هذا العالم الزائل؛ إذ كان المشركون يَسخَرون من المؤمنين، ويَلمِزونهم، ويستضعفونهم، وكيف انقلب الحالُ في العالم الأبدي». "التحرير والتنوير" لابن عاشور (30 /188).