ترجمة سورة النازعات

Ali Muhsin Al - Swahili translation

ترجمة معاني سورة النازعات باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation.

An-Nazi'at


Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,

Na kwa wanao toa kwa upole,

Na wanao ogelea,

Wakishindana mbio,

Wakidabiri mambo.

Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,

Kifuate cha kufuatia.

Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,

Macho yatainama chini.

Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?

Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?

Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!

Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,

Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!

Je! Imekufikia hadithi ya Musa?

Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:

Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.

Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?

Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.

Basi alimwonyesha Ishara kubwa.

Lakini aliikadhibisha na akaasi.

Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.

Akakusanya watu akanadi.

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.

Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.

Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.

Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!

Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.

Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.

Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.

Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,

Na milima akaisimamisha,

Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.

Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,

Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,

Basi ama yule aliye zidi ujeuri,

Na akakhiari maisha ya dunia,

Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!

Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,

Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!

Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?

Una nini wewe hata uitaje?

Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.

Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.

Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
سورة النازعات
معلومات السورة
الكتب
الفتاوى
الأقوال
التفسيرات

سورة (النَّازعات) من السُّوَر المكية، وقد افتُتحت بذكرِ الملائكة التي تَنزِع الأرواح؛ ليبعثَ اللهُ الناس بعد ذلك في يوم الطامَّة الكبرى؛ ليكونَ من اتقى في الجِنان، ويذهبَ من طغى وآثر الحياةَ الدنيا إلى الجحيم مأواه، وقد ذكَّرت السورةُ الكريمة بنِعَمِ الله على خَلْقه وقوَّته وقهره بعد أن بيَّنتْ إقامةَ الحُجَّة على الكافرين، كما أقام موسى عليه السلام الحُجَّةَ على فرعون بالإبلاغ.

ترتيبها المصحفي
79
نوعها
مكية
ألفاظها
179
ترتيب نزولها
81
العد المدني الأول
45
العد المدني الأخير
45
العد البصري
45
العد الكوفي
46
العد الشامي
45

- قوله تعالى: {يَسْـَٔلُونَكَ عَنِ اْلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَىٰهَا ٤٢ فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَىٰهَآ} [النازعات: 42-43]:

عن عائشةَ رضي الله عنها، قالت: «كان النبيُّ صلى الله عليه وسلم يُسألُ عن الساعةِ حتى أُنزِلَ عليه: {يَسْـَٔلُونَكَ عَنِ اْلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَىٰهَا ٤٢ فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَىٰهَآ} [النازعات: 42-43]». أخرجه الحاكم (3895).

* سورة (النَّازعات):

سُمِّيت سورة (النَّازعات) بذلك؛ لافتتاحها بقَسَمِ الله بـ(النَّازعات)؛ وهم: الملائكةُ الذين ينتزعون أرواحَ بني آدم.

1. مَشاهد اليوم الآخِر (١-١٤).

2. قصة موسى عليه السلام مع فرعون (١٥-٢٦).

3. لفتُ النظر إلى خَلْقِ السموات والأرض (٢٧-٣٣).

4. أحداث يوم القيامة (٣٤-٤١).

5. سؤال المشركين عن وقتِ الساعة (٤٢-٤٦).

ينظر: "التفسير الموضوعي لسور القرآن الكريم" لمجموعة من العلماء (9 /23).

يقول ابنُ عاشور رحمه الله: «اشتملت على إثباتِ البعث والجزاء، وإبطال إحالة المشركين وقوعَه، وتهويلِ يومه، وما يعتري الناسَ حينئذٍ من الوَهَلِ، وإبطال قول المشركين بتعذُّرِ الإحياء بعد انعدام الأجساد». "التحرير والتنوير" لابن عاشور (30 /59).