ترجمة سورة الواقعة

Ali Muhsin Al - Swahili translation

ترجمة معاني سورة الواقعة باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation.

Al-Waki'ah


Litakapo tukia hilo Tukio

Hapana cha kukanusha kutukia kwake.

Literemshalo linyanyualo,

Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,

Na milima itapo sagwasagwa,

Iwe mavumbi yanayo peperushwa,

Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-

Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?

Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?

Na wa mbele watakuwa mbele.

Hao ndio watakao karibishwa

Katika Bustani zenye neema.

Fungu kubwa katika wa mwanzo,

Na wachache katika wa mwisho.

Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.

Wakiviegemea wakielekeana.

Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,

Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.

Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.

Na matunda wayapendayo,

Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.

Na Mahurulaini,

Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.

Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.

Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,

Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.

Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?

Katika mikunazi isiyo na miba,

Na migomba iliyo pangiliwa,

Na kivuli kilicho tanda,

Na maji yanayo miminika,

Na matunda mengi,

Hayatindikii wala hayakatazwi,

Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.

Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,

Na tutawafanya vijana,

Wanapendana na waume zao, hirimu moja.

Kwa ajili ya watu wa kuliani.

Fungu kubwa katika wa mwanzo,

Na fungu kubwa katika wa mwisho.

Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?

Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,

Na kivuli cha moshi mweusi,

Si cha kuburudisha wala kustarehesha.

Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.

Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,

Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?

Au baba zetu wa zamani?

Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho

Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.

Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,

Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.

Na kwa mti huo mtajaza matumbo.

Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.

Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.

Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.

Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?

Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?

Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?

Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi

Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.

Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?

Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?

Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?

Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,

Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;

Bali sisi tumenyimwa.

Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?

Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?

Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?

Je! Mnauona moto mnao uwasha?

Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?

Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.

Basi naapa kwa maanguko ya nyota,

Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!

Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,

Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.

Hapana akigusaye ila walio takaswa.

Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?

Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?

Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,

Na nyinyi wakati huo mnatazama!

Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.

Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,

Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,

Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.

Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,

Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.

Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,

Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,

Na kutiwa Motoni.

Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.
سورة الواقعة
معلومات السورة
الكتب
الفتاوى
الأقوال
التفسيرات

سورة (الواقعة) من السُّوَر المكية، نزلت بعد سورة (طه)، وقد جاءت بتذكيرِ الناس بوقوع يوم القيامة؛ للدَّلالة على عظمة الله عز وجل، وترهيبًا لهم من مخالفة أوامره، ودعوةً لهم إلى اتباع الدِّين الحق وتركِ الباطل، وخُتمت السورة الكريمة بتعظيمِ القرآن، وصدقِ أخباره وما جاء به، وقد أُثر عن النبي صلى الله عليه وسلم قراءتُه لها في صلاة الفجر.

ترتيبها المصحفي
56
نوعها
مكية
ألفاظها
380
ترتيب نزولها
46
العد المدني الأول
99
العد المدني الأخير
99
العد البصري
97
العد الكوفي
96
العد الشامي
99

* قوله تعالى: {فَلَآ أُقْسِمُ بِمَوَٰقِعِ اْلنُّجُومِ ٧٥ وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ ٧٦ إِنَّهُۥ لَقُرْءَانٞ كَرِيمٞ ٧٧ فِي كِتَٰبٖ مَّكْنُونٖ ٧٨ لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا اْلْمُطَهَّرُونَ ٧٩ تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ اْلْعَٰلَمِينَ ٨٠ أَفَبِهَٰذَا اْلْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ ٨١ وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ} [الواقعة: 75-82]:

عن عبدِ اللهِ بن عباسٍ رضي الله عنهما، قال: «مُطِرَ الناسُ على عهدِ النبيِّ ﷺ، فقال النبيُّ ﷺ: «أصبَحَ مِن الناسِ شاكرٌ، ومنهم كافرٌ، قالوا: هذه رحمةُ اللهِ، وقال بعضُهم: لقد صدَقَ نَوْءُ كذا وكذا»، قال: فنزَلتْ هذه الآيةُ: {فَلَآ أُقْسِمُ بِمَوَٰقِعِ اْلنُّجُومِ} [الواقعة: 75]، حتى بلَغَ: {وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ} [الواقعة: 82]». أخرجه مسلم (٧٣).

* سورة (الواقعة):

سُمِّيت هذه السورة بـ(الواقعة)؛ لافتتاحِها بهذا اللفظ، ولتسميةِ النبيِّ صلى الله عليه وسلم لها بذلك:

عن أبي بكرٍ الصِّدِّيقِ رضي الله عنه، قال: «سألتُ رسولَ اللهِ ﷺ: ما شيَّبَكَ؟ قال: «سورةُ هودٍ، والواقعةِ، و{عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ}، و{إِذَا اْلشَّمْسُ كُوِّرَتْ}»». أخرجه الترمذي (٣٢٩٧).

و(الواقعةُ): اسمٌ من أسماءِ يوم القيامة.

* سورة (الواقعة) من السُّوَر التي شيَّبتْ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم:

عن أبي بكرٍ الصِّدِّيقِ رضي الله عنه، قال: «سألتُ رسولَ اللهِ ﷺ: ما شيَّبَكَ؟ قال: «سورةُ هودٍ، والواقعةِ، و{عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ}، و{إِذَا اْلشَّمْسُ كُوِّرَتْ}»». أخرجه الترمذي (٣٢٩٧).

* أُثِر عن النبي صلى الله عليه وسلم قراءتُه لسورة (الواقعة) في صلاة الفجر:

عن جابرِ بن سَمُرةَ رضي الله عنه، قال: «كان رسولُ اللهِ ﷺ يُصلِّي الصَّلواتِ كنَحْوٍ مِن صلاتِكم التي تُصَلُّون اليومَ، ولكنَّه كان يُخفِّفُ، كانت صَلاتُه أخَفَّ مِن صَلاتِكم، وكان يَقرأُ في الفجرِ الواقعةَ، ونحوَها مِن السُّوَرِ». أخرجه أحمد (٢٠٩٩٥).

1. تحقيق القيامة (١-٥٦).

2. دلائلُ البعث والجزاء (٥٧-٧٤).

3. تعظيم القرآن، وصدقُ أخباره (٧٥-٩٦).

ينظر: "التفسير الموضوعي لسور القرآن الكريم" لمجموعة من العلماء (7 /598).

مقصدُ سورة (الواقعة) هو التذكيرُ بوقوع يوم القيامة وهَوْلِه، ووصفُ ما يحدُثُ به؛ لتخويف الناس وترهيبهم من معصية الله عز وجل ومخالفة أمره، وفي ذلك دعوةٌ لهم للرجوع إلى الحق، والاستجابة لأمر الله.

ويُبيِّن ابن عاشور محورَها فيقول: «هو التذكيرُ بيوم القيامة، وتحقيق وقوعه.

ووصفُ ما يَعرِض لهذا العالَمِ الأرضي عند ساعة القيامة.

ثم صفة أهل الجنة وبعض نعيمهم.

وصفة أهل النار وما هم فيه من العذاب، وأن ذلك لتكذيبهم بالبعث.

وإثبات الحشر والجزاء.

والاستدلال على إمكان الخَلْق الثاني بما أبدعه الله من الموجودات بعد أن لم تكن.

والاستدلال بدلائل قدرة الله تعالى.

والاستدلال بنزعِ الله الأرواحَ من الأجساد والناس كارهون لا يستطيع أحدٌ مَنْعَها من الخروج، على أن الذي قدَرَ على نزعها بدون مُدافعٍ قادرٌ على إرجاعها متى أراد على أن يُمِيتَهم.

وتأكيد أن القرآن منزلٌ من عند الله، وأنه نعمةٌ أنعم الله بها عليهم فلم يشكروها، وكذَّبوا بما فيه». "التحرير والتنوير" لابن عاشور (27 /280).